Sunday, 22 September 2013

WAzIRI WA USALAMA KENYA AMESEMA WATU 59 WAMEFARIKI NA WENGINE 175 KUJERUHIWA KATIKA SHAMBULIO LA KIGAIDI WESTGATE



Serikali ya Kenya kupitia kwa waziri wake wa usalama Joseph Ole Lenku imesema kuwa watu 59 wamefariki katika shambulizi la kigaidi lililofanywa na wanamgambo wa Al Shabaab na wengine 175 kujeruhiwa.

Waziri Ole Lenku amesema kuwa idadi ya magaidi walio ndani ya jengo hilo ni kati ya kumi na kumi na tano na haijulikani ikiwa wanawazulia waathiriwa au waathiriwa wamejificha katika sehemu mbali mbali za jumba la Westgate.


Kuna taarifa kuwa wanamgambo hao wako ndani ya duka moja kubwa katika jengo hilo.
Rais Kenyatta anasema kuwa baadhi ya waliofariki ni jamaa zake. Miongoni mwa waliofariki pia ni mwanadiplomasia wa Canada na raia wawili wa Ufaransa. 

Rais Kenyatta anasema kuwa wale waliohusika lazima wakabiliwe na mkono wa sheria.
Jamaa na marafiki waliofika kujua hali ya jamaa zao wamezuiwa kuingia ndani ya jengo hilo. Wengi wa waathiriwa walifariki kutokana na majeraha yao.




 Baadhi ya wananchi wakikimbia wakati mashambulizi yakiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: only a member of this blog may post a comment.